التين
The Fig • 8 ayahs • Meccan
بِسْمِ ٱللَّهِ ٱلرَّحْمَٰنِ ٱلرَّحِيمِ
1Ninaapa kwa tini na zaituni!
2Na kwa Mlima wa Sinai!
3Na kwa Mji huu wenye amani mno!
4Bila ya shaka tumemuumba mtu kwa umbo lilio bora kabisa.
5Kisha tukamrudisha kuwa chini kuliko walio chini!
6Isipokuwa wale walioamini na wakatenda mema, hao watapata ujira usiokwisha.
7Basi ni kipi baadaye kitakachokukukadhibishia malipo?
8Kwani Mwenyezi Mungu si muadilifu zaidi kuliko wote wanaohukumu?