الفاتحة
The Opening • 7 ayahs • Meccan
1Kwa jina la Mwenyezi Mungu, Mwingi wa rehema, Mwenye kurehemu.
2Sifa njema zote ni za Mwenyezi Mungu, Mola Mlezi wa walimwengu.[1]
3Mwingi wa rehema, Mwenye kurehemu.[1]
4Mmiliki wa Siku ya Malipo.
5Ni Wewe tu tunayeabudu, na ni Wewe tu tunayeomba msaada.
6Tuongoe kwenye njia iliyonyooka.
7Njia ya wale uliowaneemesha. Siyo ya wale waliokasirikiwa, wala waliopotea.