Al-Inshiqaq

الانشقاق

The Splitting Open25 ayahsMeccan

بِسْمِ ٱللَّهِ ٱلرَّحْمَٰنِ ٱلرَّحِيمِ

إِذَا ٱلسَّمَآءُ ٱنشَقَّتۡ﴿١

1Itakapochanika mbingu.

وَأَذِنَتۡ لِرَبِّهَا وَحُقَّتۡ﴿٢

2Na ikamsikiliza Mola wake Mlezi, na ikapasiwa kumsikiliza.

وَإِذَا ٱلۡأَرۡضُ مُدَّتۡ﴿٣

3Na ardhi itakapotanuliwa.

وَأَلۡقَتۡ مَا فِيهَا وَتَخَلَّتۡ﴿٤

4Na kuvitoa vilivyokuwa ndani yake, ikawa tupu.

وَأَذِنَتۡ لِرَبِّهَا وَحُقَّتۡ﴿٥

5Na ikamsikiliza Mola wake Mlezi, na ikapasiwa kumsikiliza.

يَٰٓأَيُّهَا ٱلۡإِنسَٰنُ إِنَّكَ كَادِحٌ إِلَىٰ رَبِّكَ كَدۡحٗا فَمُلَٰقِيهِ﴿٦

6Ewe mtu! Hakika wewe unafanya matendo kwa juhudi kumwendea Mola wako Mlezi, basi utamkuta.

فَأَمَّا مَنۡ أُوتِيَ كِتَٰبَهُۥ بِيَمِينِهِۦ﴿٧

7Ama atakayepewa daftari lake kwa mkono wa kulia.

فَسَوۡفَ يُحَاسَبُ حِسَابٗا يَسِيرٗا﴿٨

8Basi huyo atahisabiwa hisabu nyepesi.

وَيَنقَلِبُ إِلَىٰٓ أَهۡلِهِۦ مَسۡرُورٗا﴿٩

9Na arudi kwa ahali zake na furaha.

وَأَمَّا مَنۡ أُوتِيَ كِتَٰبَهُۥ وَرَآءَ ظَهۡرِهِۦ﴿١٠

10Na ama atakayepewa daftari lake kwa nyuma ya mgongo wake.

فَسَوۡفَ يَدۡعُواْ ثُبُورٗا﴿١١

11Basi huyo ataomba kuteketea.

وَيَصۡلَىٰ سَعِيرًا﴿١٢

12Na ataingia Motoni.

إِنَّهُۥ كَانَ فِيٓ أَهۡلِهِۦ مَسۡرُورًا﴿١٣

13Hakika alikuwa furahani kati ya jamaa zake.

إِنَّهُۥ ظَنَّ أَن لَّن يَحُورَ﴿١٤

14Huyo hakika alidhani kuwa hatarejea tena.

بَلَىٰٓۚ إِنَّ رَبَّهُۥ كَانَ بِهِۦ بَصِيرٗا﴿١٥

15Kwani? Hakika Mola wake Mlezi alikuwa akimwona vyema!

فَلَآ أُقۡسِمُ بِٱلشَّفَقِ﴿١٦

16Basi ninaapa kwa wekundu wa jua linapokuchwa.

وَٱلَّيۡلِ وَمَا وَسَقَ﴿١٧

17Na kwa usiku na unavyovikusanya.

وَٱلۡقَمَرِ إِذَا ٱتَّسَقَ﴿١٨

18Na kwa mwezi unapopevuka.

لَتَرۡكَبُنَّ طَبَقًا عَن طَبَقٖ﴿١٩

19Lazima mtapanda tabaka kwa tabaka!

فَمَا لَهُمۡ لَا يُؤۡمِنُونَ﴿٢٠

20Basi wana nini hawaamini?

وَإِذَا قُرِئَ عَلَيۡهِمُ ٱلۡقُرۡءَانُ لَا يَسۡجُدُونَۤ۩﴿٢١

21Na wanaposomewa Qur-ani hawasujudu?

بَلِ ٱلَّذِينَ كَفَرُواْ يُكَذِّبُونَ﴿٢٢

22Bali waliokufuru wanakanusha tu.

وَٱللَّهُ أَعۡلَمُ بِمَا يُوعُونَ﴿٢٣

23Na Mwenyezi Mungu anajua wanayoyadhamiria.

فَبَشِّرۡهُم بِعَذَابٍ أَلِيمٍ﴿٢٤

24Basi wabashirie adhabu chungu!

إِلَّا ٱلَّذِينَ ءَامَنُواْ وَعَمِلُواْ ٱلصَّٰلِحَٰتِ لَهُمۡ أَجۡرٌ غَيۡرُ مَمۡنُونِۭ﴿٢٥

25Isipokuwa wale walioamini na wakatenda mema; hao watakuwa na ujira usiomalizika.

RELATED SURAHS